| Waziri wa Fedha, Saada Mkuya |
MWANGAZA WA HABARI
Alhamisi, 30 Oktoba 2014
Jumatano, 29 Oktoba 2014
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA MWEZI YA WANAWAKE WAJASILIAMALI (MOWE)
Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Mohammed Gharib Bilal,jana amekua mgeni rasmi katika maonyesho ya mwezi wa wanawake wajasiliamali (WOMA) uliofanyika jijini Dar es salaam ukiwa na lengo la kuwatambua wanawake wanaojishughurisha katika biashara mbalimbali ili kuwahamasisha wanawake wengine ambao nao wanatamani kuwa wajasiliamali na wale wasijishughulisha kuasishika.

Katika ufunguzi huo Dkt Bilali ametembelea mabanda ya wanawake hao na kujionea biashara zinazofanywa na wajasiriamali huku akionekana kurizishwa na kazi zao pia aliwasapoti kwa kununua baadhi za bidhaa walizoziuza na kuataka kuendeleza bidii katika biashara zao ili na wao wasiwe tegemezi.

Pia maonyesho hayo yameshuhudiwa na viongozi mbalimbali ambao nao walijaribu kuzidi kuwahamasisha wanawake hao wajasiliamali kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kupata maendeleo yao na taifa kwa ujumla na si kusubilia maonyesho kama kutengeneza bidhaa zao.
![]() |
| Makamu wa Rais Dkt Bilali katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali na wageni waalikwa katika maonyesho hayo. |
WANAWAKE WAMEHAMASISHWA KUTUMIA FULSA ILIYOPO KATIKA SEKTA YA BAHARI
Wanawake wameaswa kutumia fursa
iliyopo katika sekta ya bahari kwa kupata elimu na mafunzo ya sekta hiyo
ambayo ni msingi wao katika kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia
ukuaji sayansi na teknolojia inayoongezeka kwa kasi duniani.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa
Usalama wa Mazingira Majini Tumpe Mwaijande kutoka Wizara ya Uchukuzi
kwaniaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Shaaban Mwinjaka wakati wa
ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Umoja wanawake walio katika Sekta ya
masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) ulifanyika jana Dar es salaam.
![]() |
| Mwenyekiti wa WOMASA kutoka Mauritius Bi. Meenaksi Bhirugnath Bhookun akitoa mada wakati wa ufunguzi wa mkutano huo |
Katika mkutano huo wa siku nne
ambao umeanza leo oktoba 28 na unatarajiwa kumalizika Oktoba 31 mwaka
huu, mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo mpango mkakati wa WOMESA
kuhusu ushiriki wa wanawake katika masuala ya sekta ya bahari katika
nchi wanachama.
Kwa upande wake Mkurugenzi
Msaidizi kutoka Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Mambo ya Bahari
(IMO) Pamela Tansey amesema kuwa WOMESA imekuwa msatari wa mbele katika
kumwendeleza mwanamke kwenye sekta ya bahari.
Pamela amesisitiza kuwa wajumbe
wa mkutano huo ni vema waelewe na kusimamia dira ya WOMESA ambayo lengo
lake ni kuwawezesha wanawake kupata ajira katika sekta ya masuala ya
bahari kwa njia ya kupta elimu na mafunzo katika kuendeleza taaluma yao
juu ya masuala ya bahari.
Mkutano huo wa WOMESA
unajumuisha wajumbe 52 kutoka nchi mbalimbali wanachama zikiwamo
Ethiopia, Namibia, Komoro, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Mauritius na
Kenya.
Nchi nyingine ni Angola, Sudani,
Lesotho, Uganda, Somalia, Eritrea, Botswana, Rwanda, Madagaska, Afrika
Kusini, Msumbiji, Burundi, Malawi, Djibout, Zimbabwe na wenyeji
Tanzania.
Mkatano huo wa siku nne
unafanyika nchini chini ya ufadhili wa Mamlaka ya Bandari Tanzania
(TPA), Taasisi ya Masuala ya Bahari Tanzania (DMI), shirika la mfuko
wa hifadhi ya jamii (NSSF) kwa kushirikiana na Shirika la Kimataifa
linaloshughulikia Mambo ya Bahari (IMO) na Shirika la Kimataifa la
Maendeleo (UNDP).
Jumanne, 28 Oktoba 2014
MWENYEKITI MWENZA WA TAASISI YA BILL AND MELINDA GATES ASEMA WAWEZESHENI WANAWAKE KUISAIDIA AFRIKA
Licha ya uwepo wa fikra tofauti juu ya maendeleo kwa wanawake mfadhili Melinda Gates, anaamini ukitaka kuisaidia Afrika kwanza anza na wanawake kwa kuwa ni ufunguo katika kukuza uchumi na maendeleo Afrika
Bi Melinda akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Paris hivi karibuni , kuhusu mradi wa kuchangisha fedha kwa ajili ya wanawake na wasichana alisema kuwawezesha wanawake ni miongoni mwa malengo yenye kipaumbele chenye nguvu katika taasisi ya Bill na Melinda Gates katika mkakati wa kuwasaidia watu katika nchi zinazoendelea kuwa huru katika nyanja ya afya, uzazi wa mpango na hali ngumu ya maamuzi kuhusu uchumi.
Hii ni kutokana na kuwa na ushahidi unaoonyesha wanawake barani Afrika , Asia na Amerika kusini wanauwezo mkubwa wa kuweka akiba ya fedha na kuirudisha katika matumizi ya familia kuliko wanaume wanavyofanya. Ambapo kuweka akiba huko kuna msaada kwa familia ya mwanamke na jamii kwa ujumla hali ambayo inashawishi kuwasaidia wanawake na wasichana katika maendeleo.
Kama kuna haja ya kukuza uchumi barani Afrika ni lazima uanze na wanawake licha ya kuwa mengi yanasemwa kuhusu mahitaji ya kuwawezesha wanawake ikiwemo ya kuzingatia katika kupunguza idadi ya uzazi na kuongeza jitihada za afya ya uzazi ambayo ni mkakati wa pili kati ya nane wa maendeleo ya milenia uliowekwa mwaka 2000 na jitihada kubwa zimefanywa kulisogeza hilo mbele.
Melinda amefafanua kuwa vifo vinavyotokana na uzazi vimepungua mara tatu kwa miaka 30 iliyopita na vifo vya watoto wachanga vimepungua kwa nusu ya ilivyokuwa kabla ya mpango huu. Makundi ya misaada yanafanya kazi kwa mpango mpya wa Milenia wenye lengo la kukuza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake ambako kutasaidia kupunguza umasikini na njaa.
Kwa mujibu wa ripoti ya kilimo na chakula ya Umoja wa mataifa ya mwaka 2010 -2011, kama wanawake watashirikishwa katika kilimo kwa nchi zinazoendelea kutaongeza mazao na hatimae kutasaidia kupunguza idadi ya watu wanaokosa chakula kwa asilimia 12 mpaka 17.
MWANAMKE APIGWA NA MUMEWE HADI KUFA HUKO MKOANI MOROGORO
Bado ukatiri unaofanywa na wanaume kwa wake zao unaenderea kuripotiwa huku ikiwa jamii ikitahayari kuona Katibu mkuu wa CCM Mkoa wa morogoro Bi. Rozina kopa ameuwawa baada ya
kupigwa na mumewe huku chanzo cha kupigwa kwake adi kufa bado
hakijafahamika.
Marehemu bi. Rozina kabla ya kifo chake inasemekana baada ya kukorofishana na mumewe nyumbani aliamua kuondoka ili akwepe ugomvi kuenderea ndipo mtuhumiwa wa mauaji hayo Hamis Tata ambaye ni mume wa marehemu alimsaka tena mkewe na ndipo alipomkuta kwenye bar ya mafiga bar na kuanza kumpiga.
Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo bwana mmoja aliyefahamika kwa jina la Rajabu alisema yeye ameshuhudia tukio hilo na alijaribu kumzuia mtuhumiwa kumpiga huku marehemu akionekana anavuja sana damu hasa sehemu za usoni na ndipo mtuhumiwa alimuacha kumpiga mkewe.
Kwa upande wa ndugu wa marehemu wamesema ndugu yao baada ya kupigwa sana pale bar waliporudi nyumbani mtuhumiwa aliendelea kumpiga mkewe na kumuingilia kimapenzi bila idhini yake
kabla mauti haijamkuta walimkimbiza hospitali ya mkoa uku akiwa akilalamika kifua kumuuma sana .
Naye kamanda wa polisi mkoani morogoro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na adi sasa wanamshikiria bw. Hamis Tata kwa tuhuma za mauaji.
Hili ni moja ya tukio baya ambalo bado linazidi kuongeza idadi ya vifo vya kinyama vinavyofanywa na wanaume kwa wake zao na hatimaye mwili wa Bi Rozina Tata umezikwa katika makaburi ya kora huko mkoani Morogoro.
Marehemu bi. Rozina kabla ya kifo chake inasemekana baada ya kukorofishana na mumewe nyumbani aliamua kuondoka ili akwepe ugomvi kuenderea ndipo mtuhumiwa wa mauaji hayo Hamis Tata ambaye ni mume wa marehemu alimsaka tena mkewe na ndipo alipomkuta kwenye bar ya mafiga bar na kuanza kumpiga.
Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo bwana mmoja aliyefahamika kwa jina la Rajabu alisema yeye ameshuhudia tukio hilo na alijaribu kumzuia mtuhumiwa kumpiga huku marehemu akionekana anavuja sana damu hasa sehemu za usoni na ndipo mtuhumiwa alimuacha kumpiga mkewe.
Kwa upande wa ndugu wa marehemu wamesema ndugu yao baada ya kupigwa sana pale bar waliporudi nyumbani mtuhumiwa aliendelea kumpiga mkewe na kumuingilia kimapenzi bila idhini yake
kabla mauti haijamkuta walimkimbiza hospitali ya mkoa uku akiwa akilalamika kifua kumuuma sana .
Naye kamanda wa polisi mkoani morogoro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na adi sasa wanamshikiria bw. Hamis Tata kwa tuhuma za mauaji.
Hili ni moja ya tukio baya ambalo bado linazidi kuongeza idadi ya vifo vya kinyama vinavyofanywa na wanaume kwa wake zao na hatimaye mwili wa Bi Rozina Tata umezikwa katika makaburi ya kora huko mkoani Morogoro.
SCANDAVIA YAONGOZA UWIANO WA KIJINSIA
Katika
ripoti mpya ya mwaka iliyoitoa Jukwaa la kiuchumi duniani inaonyesha nchi za Scandavia zinaongoza kwa uwiano wa kijinsia kwa kuangaza fulsa kwa wanawake katika nchi 142 huku nchi za Afrika zikiongozwa na
Rwanda.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika ripoti hiyo, Kwanza, wanawake wanafanyakazi na kulipwa malipo sawa kwa kazi iliyosawa na nafasi ya kupata elimu.
Maeneo mengine yaliyozingatiwa ni kweli wanawake wanaruhusiwa kushiriki katika masuala ya kisiasa haswa katika ngazi za juu, kuweza kushika nafasi za ubunge na hata madaraka ya juu zaidi Nchi zilizotajwa katika ripoti hiyo kuongoza ni Iceland ikifuatiwa na Norway, Finland, Sweden, Denmark.
Phillipines nchi iliyo katika bara Asia imeshika nafasi ya tisa. Rwanda imeibuka kidedea kwa kuweza kuingia katika 10 bora ya nchi hizo 142, ambazo zilifanyiwa utafiti na pia kuwa nchi ya kwanza ya Afrika na zinazoendelea kuweza kushika nafasi ya kwanza katika ripoti hiyo.
Mafanikio ya Rwanda yanatokana na uwezo wa kupata huduma za afya na elimu, lakini pia, yanaangazia idadi kubwa ya wanawake wanaoshika nafasi za uwaziri.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo mafanikio ya wanawake yanazidi kuonekana, kwani sasa kuna asilimia 26 zaidi ya wanawake wabunge duniani kote na asilimia 50 zaidi ya wanawake mawaziri kushinda ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.
Utafiti huo uliofanywa umeonesha pia kuwa pengo kubwa katika usawa wa kijinsia lipo katika nchi za Chad, Pakistan na Yemen, ambako hakuna mabadiliko na mwaka uliopita.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika ripoti hiyo, Kwanza, wanawake wanafanyakazi na kulipwa malipo sawa kwa kazi iliyosawa na nafasi ya kupata elimu.
Maeneo mengine yaliyozingatiwa ni kweli wanawake wanaruhusiwa kushiriki katika masuala ya kisiasa haswa katika ngazi za juu, kuweza kushika nafasi za ubunge na hata madaraka ya juu zaidi Nchi zilizotajwa katika ripoti hiyo kuongoza ni Iceland ikifuatiwa na Norway, Finland, Sweden, Denmark.
Phillipines nchi iliyo katika bara Asia imeshika nafasi ya tisa. Rwanda imeibuka kidedea kwa kuweza kuingia katika 10 bora ya nchi hizo 142, ambazo zilifanyiwa utafiti na pia kuwa nchi ya kwanza ya Afrika na zinazoendelea kuweza kushika nafasi ya kwanza katika ripoti hiyo.
Mafanikio ya Rwanda yanatokana na uwezo wa kupata huduma za afya na elimu, lakini pia, yanaangazia idadi kubwa ya wanawake wanaoshika nafasi za uwaziri.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo mafanikio ya wanawake yanazidi kuonekana, kwani sasa kuna asilimia 26 zaidi ya wanawake wabunge duniani kote na asilimia 50 zaidi ya wanawake mawaziri kushinda ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.
Utafiti huo uliofanywa umeonesha pia kuwa pengo kubwa katika usawa wa kijinsia lipo katika nchi za Chad, Pakistan na Yemen, ambako hakuna mabadiliko na mwaka uliopita.
Jumatatu, 27 Oktoba 2014
MAHAFALI YA PILI YA SHULE YA WAMA NAKAYAMA YAFANYIKA HUKU UBALOZI WA JAPANI WAISAIDIA SHULE HIYO SH. MILIONI 800
Ubalozi
wa japan kupitia wizara ya Mambo ya Nje umetoa msaada wa kiasi cha
fedha cha sh. Milioni 800 ambazo ni sawa na dola za Kimarekani 500,000
kwa ajiri ya kusaidia Shule ya Sekondari ya wasichana wanaoishi katika
maisha magumu na hatarishi ya WAMA Nakayama, iliyopo wilayani Rufiji
mkoani pwani.
Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa japan nchini Kazuyoshi Matsu Naga wakati wa sherehe za mahafari ya pili ya shule hiyo yaliyofanyika jana na kuhudhuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro ambaye alikua mgeni rasmi baadhi ya viongozi wengine wakiwemo baadhi ya wake wa wageni wengine mbalimbali.
Akizungumzia kuhusu matarajio ya WAMA kutokana shule hiyo, alisema kutoa wataalamu wa nyanja zote , ikiwemo fani ya sayansi . Hivyo aliwataka kuongeza bidii katika masomo ya sayansi. Alisema WAMA itaendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hadi watakapofikia hatua ya mwisho.
Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa japan nchini Kazuyoshi Matsu Naga wakati wa sherehe za mahafari ya pili ya shule hiyo yaliyofanyika jana na kuhudhuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro ambaye alikua mgeni rasmi baadhi ya viongozi wengine wakiwemo baadhi ya wake wa wageni wengine mbalimbali.
![]() |
| Waziri wa Katiba naSheria Dkt Asha Rose Migiro (katikati) Akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendereo WAMA Mama Salma Kikwete pamoja na Kaimu balozi wa Japani. |
Kwa upande wake, Dkt. Migiro, ambaye alikuwa mgeni rasmi
katika sherehe hizo, aliwataka wadau mbalimbali kuendelea kumsaidia
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma Kikwete
katika kusaidia wanafunzi hao ili kupanua fursa za watoto wa kike
kielimu
Naye Mke wa Rais Mama Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka wanafunzi hao
kutumia nafasi ya kusoma bidii ili waweze kufaulu hatimaye kushika
nafasi mbalimbali za uongozi kama Dkt.
Akizungumzia kuhusu matarajio ya WAMA kutokana shule hiyo, alisema kutoa wataalamu wa nyanja zote , ikiwemo fani ya sayansi . Hivyo aliwataka kuongeza bidii katika masomo ya sayansi. Alisema WAMA itaendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hadi watakapofikia hatua ya mwisho.
![]() |
| Wahitimu wa elimu ya sekondari kidato cha nne katika shure hiyo ya WAMA wakati wa sherehe yao ya kumaliza |
Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa Tamisemi (TAMISEMI) Hawa Ghasia aliwapongeza walimu
wa shule hiyo kwa bidii zao ambao zimeifanya shule hiyo kuongeza
katika wilaya hiyo.
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)




