Jumatano, 29 Oktoba 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA MWEZI YA WANAWAKE WAJASILIAMALI (MOWE)

Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Mohammed Gharib Bilal,jana amekua mgeni rasmi katika maonyesho ya mwezi wa wanawake wajasiliamali (WOMA) uliofanyika jijini Dar es salaam ukiwa na lengo la kuwatambua wanawake wanaojishughurisha katika biashara mbalimbali ili kuwahamasisha wanawake wengine ambao nao wanatamani kuwa wajasiliamali na wale wasijishughulisha kuasishika.

 9

Katika ufunguzi huo Dkt Bilali ametembelea mabanda ya wanawake hao na kujionea biashara zinazofanywa na wajasiriamali huku akionekana kurizishwa na kazi zao pia aliwasapoti kwa kununua baadhi za bidhaa walizoziuza na kuataka kuendeleza bidii katika biashara zao ili na wao wasiwe tegemezi.

 4

 Pia maonyesho hayo yameshuhudiwa na viongozi  mbalimbali ambao nao walijaribu kuzidi kuwahamasisha wanawake hao wajasiliamali kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kupata maendeleo yao na taifa kwa ujumla na si kusubilia maonyesho kama kutengeneza bidhaa zao.
 
11
Makamu wa Rais Dkt Bilali katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali na wageni waalikwa katika maonyesho hayo.
 

WANAWAKE WAMEHAMASISHWA KUTUMIA FULSA ILIYOPO KATIKA SEKTA YA BAHARI

Wanawake wameaswa kutumia fursa iliyopo katika sekta ya bahari kwa kupata elimu na mafunzo ya sekta hiyo ambayo ni msingi wao katika kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia ukuaji sayansi na teknolojia inayoongezeka kwa kasi duniani.
 
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Usalama wa Mazingira Majini Tumpe Mwaijande kutoka Wizara ya Uchukuzi kwaniaba ya Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Shaaban Mwinjaka wakati wa ufunguzi wa mkutano wa mwaka wa Umoja wanawake walio katika Sekta ya masuala ya Bahari Mashariki na Kusini mwa Afrika (WOMESA) ulifanyika jana  Dar es salaam.
 

unnamed2
Mwenyekiti wa WOMASA kutoka Mauritius Bi. Meenaksi Bhirugnath Bhookun akitoa mada wakati wa ufunguzi wa mkutano huo
Akisoma hotuba kwa niaba ya Katibu Mkuu huyo, Mwaijande amewataka wajumbe wa mkutano huo (WOMESA), wawe tayari kujadili masuala yanayojenga na kukuza ushiriki wa wanawake katika sekta ya bahari katika nchi zao.
 
Katika mkutano huo wa siku nne ambao umeanza leo oktoba 28 na unatarajiwa kumalizika Oktoba 31 mwaka huu, mada mbalimbali zitajadiliwa ikiwemo mpango mkakati wa WOMESA kuhusu ushiriki wa wanawake katika masuala ya sekta ya bahari katika nchi wanachama. 
 
Kwa upande wake Mkurugenzi Msaidizi kutoka Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Mambo ya Bahari (IMO) Pamela Tansey amesema kuwa WOMESA imekuwa msatari wa mbele katika kumwendeleza mwanamke kwenye sekta ya bahari.
 
unnamed4
Picha ya pamoja ya wajumbe wa mkutano wa mwaka wa WOMASA mara baada ya ufunguzi wa mkutano huo.
Pamela amesisitiza kuwa wajumbe wa mkutano huo ni vema waelewe na kusimamia dira ya WOMESA ambayo lengo lake ni kuwawezesha wanawake kupata ajira katika sekta ya masuala ya bahari kwa njia ya kupta elimu na mafunzo katika kuendeleza taaluma yao juu ya masuala ya bahari.
 
Mkutano huo wa WOMESA unajumuisha wajumbe 52 kutoka nchi mbalimbali wanachama zikiwamo Ethiopia, Namibia, Komoro, Visiwa vya Shelisheli, Zambia, Mauritius na Kenya. 
 
Nchi nyingine ni Angola, Sudani, Lesotho, Uganda, Somalia, Eritrea, Botswana, Rwanda, Madagaska, Afrika Kusini, Msumbiji, Burundi, Malawi, Djibout, Zimbabwe na wenyeji Tanzania.
 
Mkatano huo wa siku nne unafanyika nchini chini ya ufadhili wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Taasisi ya Masuala ya Bahari Tanzania (DMI),   shirika la mfuko wa hifadhi ya jamii (NSSF) kwa kushirikiana na  Shirika la Kimataifa linaloshughulikia Mambo ya Bahari (IMO) na Shirika la Kimataifa la Maendeleo (UNDP).
 

Jumanne, 28 Oktoba 2014

MWENYEKITI MWENZA WA TAASISI YA BILL AND MELINDA GATES ASEMA WAWEZESHENI WANAWAKE KUISAIDIA AFRIKA

Licha ya uwepo wa fikra tofauti juu ya maendeleo kwa wanawake mfadhili Melinda Gates, anaamini ukitaka kuisaidia Afrika kwanza anza na wanawake kwa kuwa ni ufunguo katika kukuza uchumi na maendeleo Afrika

Burundi Landwirtschaft Kilimo cha wanawake nchini Burundi

Bi Melinda akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari mjini Paris hivi karibuni , kuhusu mradi wa kuchangisha fedha kwa ajili ya wanawake na wasichana alisema kuwawezesha wanawake ni miongoni mwa malengo yenye kipaumbele chenye nguvu katika taasisi ya Bill na Melinda Gates katika mkakati wa kuwasaidia watu katika nchi zinazoendelea kuwa huru katika nyanja ya afya, uzazi wa mpango na hali ngumu ya maamuzi kuhusu uchumi.

Hii ni kutokana na kuwa na ushahidi unaoonyesha wanawake barani Afrika , Asia na Amerika kusini wanauwezo mkubwa wa kuweka akiba ya fedha na kuirudisha katika matumizi ya familia kuliko wanaume wanavyofanya. Ambapo kuweka akiba huko kuna msaada kwa familia ya mwanamke na jamii kwa ujumla hali ambayo inashawishi kuwasaidia wanawake na wasichana katika maendeleo.

Kama kuna haja ya kukuza uchumi barani Afrika ni lazima uanze na wanawake licha ya kuwa mengi yanasemwa kuhusu mahitaji ya kuwawezesha wanawake ikiwemo ya kuzingatia katika kupunguza idadi ya uzazi na kuongeza jitihada za afya ya uzazi ambayo ni mkakati wa pili kati ya nane wa maendeleo ya milenia uliowekwa mwaka 2000 na jitihada kubwa zimefanywa kulisogeza hilo mbele.

Forbes Liste Die mächtigsten Frauen der Welt Melinda Gates Mwenyekiti mwenza wa taasisi ya Bill and Melinda Gates

Melinda amefafanua kuwa vifo vinavyotokana na uzazi vimepungua mara tatu kwa miaka 30 iliyopita na vifo vya watoto wachanga vimepungua kwa nusu ya ilivyokuwa kabla ya mpango huu. Makundi ya misaada yanafanya kazi kwa mpango mpya wa Milenia wenye lengo la kukuza usawa wa kijinsia na kuwawezesha wanawake ambako kutasaidia kupunguza umasikini na njaa.

Kwa mujibu wa ripoti ya kilimo na chakula ya Umoja wa mataifa ya mwaka 2010 -2011, kama wanawake watashirikishwa katika kilimo kwa nchi zinazoendelea kutaongeza mazao na hatimae kutasaidia kupunguza idadi ya watu wanaokosa chakula kwa asilimia 12 mpaka 17.

MWANAMKE APIGWA NA MUMEWE HADI KUFA HUKO MKOANI MOROGORO

Bado ukatiri unaofanywa na wanaume kwa wake zao unaenderea kuripotiwa huku ikiwa jamii ikitahayari kuona Katibu mkuu wa CCM Mkoa wa morogoro Bi. Rozina kopa ameuwawa baada ya kupigwa na mumewe huku chanzo cha kupigwa kwake adi kufa bado hakijafahamika.

Marehemu bi. Rozina kabla ya kifo chake inasemekana baada ya kukorofishana na mumewe nyumbani aliamua kuondoka ili akwepe ugomvi kuenderea ndipo mtuhumiwa wa mauaji hayo Hamis Tata ambaye ni mume wa marehemu alimsaka tena mkewe na ndipo alipomkuta kwenye bar ya mafiga bar na kuanza kumpiga.

Mashuhuda wa tukio hilo akiwemo bwana mmoja aliyefahamika kwa jina la Rajabu alisema yeye ameshuhudia tukio hilo na alijaribu kumzuia mtuhumiwa kumpiga huku marehemu akionekana anavuja sana damu hasa sehemu za usoni na ndipo mtuhumiwa alimuacha kumpiga mkewe.

 Kwa upande wa  ndugu wa marehemu wamesema ndugu yao baada ya kupigwa sana pale bar waliporudi nyumbani mtuhumiwa aliendelea kumpiga mkewe na kumuingilia kimapenzi bila idhini yake
kabla mauti haijamkuta walimkimbiza hospitali ya mkoa uku akiwa akilalamika kifua kumuuma sana .

Naye kamanda wa polisi mkoani morogoro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na adi sasa wanamshikiria bw. Hamis Tata kwa tuhuma za mauaji.

Hili ni moja ya tukio baya ambalo bado linazidi kuongeza idadi ya vifo vya kinyama vinavyofanywa na wanaume kwa wake zao na hatimaye mwili wa Bi Rozina Tata umezikwa katika makaburi ya kora huko mkoani Morogoro.

SCANDAVIA YAONGOZA UWIANO WA KIJINSIA

Katika ripoti mpya ya mwaka iliyoitoa Jukwaa la kiuchumi duniani inaonyesha nchi za Scandavia zinaongoza kwa uwiano wa kijinsia kwa kuangaza fulsa kwa wanawake katika nchi 142 huku nchi za Afrika zikiongozwa na Rwanda.

Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika ripoti hiyo, Kwanza, wanawake wanafanyakazi na kulipwa malipo sawa kwa kazi iliyosawa na nafasi ya kupata elimu.

Maeneo mengine yaliyozingatiwa ni kweli wanawake wanaruhusiwa kushiriki katika masuala ya kisiasa haswa katika ngazi za juu, kuweza kushika nafasi za ubunge na hata madaraka ya juu zaidi Nchi zilizotajwa katika ripoti hiyo kuongoza ni Iceland ikifuatiwa na Norway, Finland, Sweden, Denmark.

Phillipines nchi iliyo katika bara Asia imeshika nafasi ya tisa. Rwanda imeibuka kidedea kwa kuweza kuingia katika 10 bora ya nchi hizo 142, ambazo zilifanyiwa utafiti na pia kuwa nchi ya kwanza ya Afrika na zinazoendelea kuweza kushika nafasi ya kwanza katika ripoti hiyo.

Mafanikio ya Rwanda yanatokana na uwezo wa kupata huduma za afya na elimu, lakini pia, yanaangazia idadi kubwa ya wanawake wanaoshika nafasi za uwaziri.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo mafanikio ya wanawake yanazidi kuonekana, kwani sasa kuna asilimia 26 zaidi ya wanawake wabunge duniani kote na asilimia 50 zaidi ya wanawake mawaziri kushinda ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.

Utafiti huo uliofanywa umeonesha pia kuwa pengo kubwa katika usawa wa kijinsia lipo katika nchi za Chad, Pakistan na Yemen, ambako hakuna mabadiliko na mwaka uliopita.

Jumatatu, 27 Oktoba 2014

MAHAFALI YA PILI YA SHULE YA WAMA NAKAYAMA YAFANYIKA HUKU UBALOZI WA JAPANI WAISAIDIA SHULE HIYO SH. MILIONI 800

 Ubalozi wa japan kupitia wizara ya Mambo ya Nje umetoa msaada wa kiasi cha fedha cha sh. Milioni 800 ambazo ni sawa na dola za Kimarekani 500,000 kwa ajiri ya kusaidia Shule ya Sekondari ya wasichana wanaoishi katika maisha magumu na hatarishi ya WAMA Nakayama, iliyopo wilayani Rufiji mkoani pwani.

Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa japan nchini Kazuyoshi Matsu Naga wakati wa sherehe za mahafari ya pili ya shule hiyo yaliyofanyika jana na kuhudhuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro ambaye alikua mgeni rasmi baadhi ya viongozi wengine wakiwemo baadhi ya wake wa wageni wengine mbalimbali.
 
IMG_8872
Waziri wa Katiba naSheria Dkt Asha Rose Migiro (katikati)  Akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendereo WAMA Mama  Salma Kikwete  pamoja na Kaimu balozi wa Japani.
Kwa upande wake, Dkt. Migiro, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, aliwataka  wadau mbalimbali  kuendelea kumsaidia Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma  Kikwete  katika kusaidia wanafunzi hao ili kupanua fursa za watoto wa kike kielimu 
Naye Mke wa Rais Mama Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka  wanafunzi hao  kutumia nafasi ya kusoma  bidii  ili waweze kufaulu hatimaye  kushika nafasi mbalimbali  za  uongozi kama Dkt.

Akizungumzia kuhusu matarajio ya WAMA kutokana shule hiyo, alisema kutoa wataalamu wa nyanja zote , ikiwemo fani ya sayansi . Hivyo  aliwataka kuongeza bidii katika masomo ya sayansi. Alisema WAMA itaendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hadi watakapofikia hatua  ya mwisho.

3
Wahitimu wa elimu ya sekondari kidato cha nne katika shure hiyo ya WAMA  wakati wa sherehe yao ya kumaliza
 Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu,  Tawala  za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi (TAMISEMI) Hawa Ghasia aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa bidii zao ambao zimeifanya shule hiyo  kuongeza katika wilaya hiyo.