Jumanne, 21 Oktoba 2014

JOYCE KIRIA WA WANAWAKE LIVE AMSAKA MUMEWE


Mtangazaji wa kipindi cha wanawake live kinachorushwa na EATV ameamua kuandama pamoja na wanawake wenzake akiwa amewabeba watoto wake wawili waitwao Lincorn na Lingatone  na kuzungumza na waandishi wa habari  nje ya jengo la idara ya Habari Maelezo  iliopo katika mtaa wa samora jijini Dar es salaam uku akipaza sauti kuomba Rais Jakaya Kikwete na Watanzania kwa ujumla ili kusaidia kujua alipo mumewe Bw. Henry Kileo  ambaye inadaiwa kuwa ameshikiriwa na polisi




Akiwa ameonekana mwenye uzuni ameamua kupaza sauti ili kuakikisha mumewe anapatikana hii ikiwa ni ishara ya kuonyesha kutaka msaada wa mumewe katika kuhakikisha wanawalea watoto wao kwa pamoja na kuamua kuwabeba watoto wake hao

Pia katika maandamano hayo ameamua kubeba mabango yenye maneno yanayosema "mume wangu upo wapi" na mabango mengine yalisomeka "Baba yangu uko wapi?".

Maoni 1 :