Mtangazaji wa kipindi cha wanawake live kinachorushwa na EATV ameamua kuandama pamoja na wanawake wenzake akiwa amewabeba watoto wake wawili waitwao Lincorn na Lingatone na kuzungumza na waandishi wa habari nje ya jengo la idara ya Habari Maelezo iliopo katika mtaa wa samora jijini Dar es salaam uku akipaza sauti kuomba Rais Jakaya Kikwete na Watanzania kwa ujumla ili kusaidia kujua alipo mumewe Bw. Henry Kileo ambaye inadaiwa kuwa ameshikiriwa na polisi
Akiwa ameonekana mwenye uzuni ameamua kupaza sauti ili kuakikisha mumewe anapatikana hii ikiwa ni ishara ya kuonyesha kutaka msaada wa mumewe katika kuhakikisha wanawalea watoto wao kwa pamoja na kuamua kuwabeba watoto wake hao
Pia katika maandamano hayo ameamua kubeba mabango yenye maneno yanayosema "mume wangu upo wapi" na mabango mengine yalisomeka "Baba yangu uko wapi?".
noma sana
JibuFuta