Jumatatu, 27 Oktoba 2014

MAHAFALI YA PILI YA SHULE YA WAMA NAKAYAMA YAFANYIKA HUKU UBALOZI WA JAPANI WAISAIDIA SHULE HIYO SH. MILIONI 800

 Ubalozi wa japan kupitia wizara ya Mambo ya Nje umetoa msaada wa kiasi cha fedha cha sh. Milioni 800 ambazo ni sawa na dola za Kimarekani 500,000 kwa ajiri ya kusaidia Shule ya Sekondari ya wasichana wanaoishi katika maisha magumu na hatarishi ya WAMA Nakayama, iliyopo wilayani Rufiji mkoani pwani.

Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa japan nchini Kazuyoshi Matsu Naga wakati wa sherehe za mahafari ya pili ya shule hiyo yaliyofanyika jana na kuhudhuliwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Asha Rose Migiro ambaye alikua mgeni rasmi baadhi ya viongozi wengine wakiwemo baadhi ya wake wa wageni wengine mbalimbali.
 
IMG_8872
Waziri wa Katiba naSheria Dkt Asha Rose Migiro (katikati)  Akiwa na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendereo WAMA Mama  Salma Kikwete  pamoja na Kaimu balozi wa Japani.
Kwa upande wake, Dkt. Migiro, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, aliwataka  wadau mbalimbali  kuendelea kumsaidia Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma  Kikwete  katika kusaidia wanafunzi hao ili kupanua fursa za watoto wa kike kielimu 
Naye Mke wa Rais Mama Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) aliwataka  wanafunzi hao  kutumia nafasi ya kusoma  bidii  ili waweze kufaulu hatimaye  kushika nafasi mbalimbali  za  uongozi kama Dkt.

Akizungumzia kuhusu matarajio ya WAMA kutokana shule hiyo, alisema kutoa wataalamu wa nyanja zote , ikiwemo fani ya sayansi . Hivyo  aliwataka kuongeza bidii katika masomo ya sayansi. Alisema WAMA itaendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hadi watakapofikia hatua  ya mwisho.

3
Wahitimu wa elimu ya sekondari kidato cha nne katika shure hiyo ya WAMA  wakati wa sherehe yao ya kumaliza
 Waziri  wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu,  Tawala  za Mikoa na Serikali za Mitaa Tamisemi (TAMISEMI) Hawa Ghasia aliwapongeza walimu wa shule hiyo kwa bidii zao ambao zimeifanya shule hiyo  kuongeza katika wilaya hiyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni