Jumatano, 29 Oktoba 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA MAONYESHO YA MWEZI YA WANAWAKE WAJASILIAMALI (MOWE)

Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Mohammed Gharib Bilal,jana amekua mgeni rasmi katika maonyesho ya mwezi wa wanawake wajasiliamali (WOMA) uliofanyika jijini Dar es salaam ukiwa na lengo la kuwatambua wanawake wanaojishughurisha katika biashara mbalimbali ili kuwahamasisha wanawake wengine ambao nao wanatamani kuwa wajasiliamali na wale wasijishughulisha kuasishika.

 9

Katika ufunguzi huo Dkt Bilali ametembelea mabanda ya wanawake hao na kujionea biashara zinazofanywa na wajasiriamali huku akionekana kurizishwa na kazi zao pia aliwasapoti kwa kununua baadhi za bidhaa walizoziuza na kuataka kuendeleza bidii katika biashara zao ili na wao wasiwe tegemezi.

 4

 Pia maonyesho hayo yameshuhudiwa na viongozi  mbalimbali ambao nao walijaribu kuzidi kuwahamasisha wanawake hao wajasiliamali kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kupata maendeleo yao na taifa kwa ujumla na si kusubilia maonyesho kama kutengeneza bidhaa zao.
 
11
Makamu wa Rais Dkt Bilali katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa vikundi mbalimbali na wageni waalikwa katika maonyesho hayo.
 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni