Binti
wa miaka 20 aliyetambulika Riziki Haji mkazi wa Kijiji cha Kondo mkoa
wa Pwani, wilayani Bagamoyo, yupo kwenye mateso makali kutokana na
ugonjwa wa kifafa unaomsumbua kwa muda mrefu!
Riziki
ambaye aliugua ugonjwa wa kifafa akiwa na umri wa miezi nane, amekuwa
akiishi katika mazingira magumu kiasi cha kufungiwa ndani usiku na
mchana.

Aidha,
imeelezwa kipindi cha mvua na baridi binti huyo huwa katika hali mbaya
zaidi kutokana na makuti yaliyotumika kutengenezewa kibanda hayahimili
hali hizo.
Akisimulia
tukio hilo, jirani wa karibu na sehemu anayoishi Riziki kwa sharti na
kutoandika jina lake, alisema Riziki amekuwa katika maisha mabaya kwa
muda mrefu huku wazazi wake baba na mama wakitupiana mpira mtu sahihi wa
kuishi nae.
“Baba
wa Riziki yupo Zanzibar na anafahamu vizuri sana hali ya mtoto wake
lakini wala hakuna msaada anaotuma….kuna muda mama yake aliamua
kumpelekea lakini siku chache baadae alimrejesha kwa mama yake! Lakini
pamoja na kumrudisha mama pia alimkataa na wasamaria wema wakamchukua na
kuishi nae,” anasema jirani huyo.
Jirani
huyo alibainisha kuwa akiwa anaendelea na maisha kwa msamaria huyo huku
akionekana mwenye afya njema, alikuja bibi yake (mama mzazi wa mama wa
Riziki) na kumchukuwa na kwenda kuishi nae Bagamoyo ambapo siku chache
baadae alimrudisha kwa mama yake mzazi akidai ameshindwa kuishi nae.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni