Ijumaa, 24 Oktoba 2014

NI KWELI MATESO AMEUMBIWA BINADAMU ILA HUYU BINTI HAYA NI MATESO YAKE

Binti wa miaka 20 aliyetambulika Riziki Haji mkazi wa Kijiji cha Kondo mkoa wa Pwani, wilayani Bagamoyo, yupo kwenye mateso makali kutokana na ugonjwa wa kifafa unaomsumbua kwa muda mrefu!
Riziki ambaye aliugua ugonjwa wa kifafa akiwa na umri wa miezi nane, amekuwa akiishi katika mazingira magumu kiasi cha kufungiwa ndani usiku na mchana.
 

 


 

 Aidha, imeelezwa kipindi cha mvua na baridi binti huyo huwa katika hali mbaya zaidi kutokana na makuti yaliyotumika kutengenezewa kibanda hayahimili hali hizo.
Akisimulia tukio hilo, jirani wa karibu na sehemu anayoishi Riziki kwa sharti na kutoandika jina lake, alisema Riziki amekuwa katika maisha mabaya kwa muda mrefu huku wazazi wake baba na mama wakitupiana mpira mtu sahihi wa kuishi nae.
“Baba wa Riziki yupo Zanzibar na anafahamu vizuri sana hali ya mtoto wake lakini wala hakuna msaada anaotuma….kuna muda mama yake aliamua kumpelekea lakini siku chache baadae alimrejesha kwa mama yake! Lakini pamoja na kumrudisha mama pia alimkataa na wasamaria wema wakamchukua na kuishi nae,” anasema jirani huyo.
Jirani huyo alibainisha kuwa akiwa anaendelea na maisha kwa msamaria huyo huku akionekana mwenye afya njema, alikuja bibi yake (mama mzazi wa mama wa Riziki) na kumchukuwa na kwenda kuishi nae Bagamoyo ambapo siku chache baadae alimrudisha kwa mama yake mzazi akidai ameshindwa kuishi nae.
Naye Juma Amani Pazi, mwenyekiti wa eneo hilo, mbali na kukiri mazingira ya Riziki kuwa mabaya, pia alisema alikuwa hana taarifa kama katika eneo lake kuna mlemavu anayeishi katika mazingira hatari kama hayo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni