Katika
ripoti mpya ya mwaka iliyoitoa Jukwaa la kiuchumi duniani inaonyesha nchi za Scandavia zinaongoza kwa uwiano wa kijinsia kwa kuangaza fulsa kwa wanawake katika nchi 142 huku nchi za Afrika zikiongozwa na
Rwanda.
Miongoni mwa mambo yaliyozingatiwa katika ripoti hiyo,
Kwanza, wanawake wanafanyakazi na kulipwa malipo sawa kwa kazi
iliyosawa na nafasi ya kupata elimu.
Maeneo mengine
yaliyozingatiwa ni kweli wanawake wanaruhusiwa kushiriki katika masuala ya
kisiasa haswa katika ngazi za juu, kuweza kushika nafasi za ubunge na
hata madaraka ya juu zaidi Nchi zilizotajwa katika ripoti hiyo kuongoza
ni Iceland ikifuatiwa na Norway, Finland, Sweden, Denmark.
Phillipines
nchi iliyo katika bara Asia imeshika nafasi ya tisa. Rwanda imeibuka
kidedea kwa kuweza kuingia katika 10 bora ya nchi hizo 142, ambazo
zilifanyiwa utafiti na pia kuwa nchi ya kwanza ya Afrika na
zinazoendelea kuweza kushika nafasi ya kwanza katika ripoti hiyo.
Mafanikio
ya Rwanda yanatokana na uwezo wa kupata huduma za afya na elimu, lakini
pia, yanaangazia idadi kubwa ya wanawake wanaoshika nafasi za uwaziri.
Kwa
mujibu wa ripoti hiyo mafanikio ya wanawake yanazidi kuonekana, kwani
sasa kuna asilimia 26 zaidi ya wanawake wabunge duniani kote na asilimia
50 zaidi ya wanawake mawaziri kushinda ilivyokuwa miaka 10 iliyopita.
Utafiti
huo uliofanywa umeonesha pia kuwa pengo kubwa katika usawa wa kijinsia
lipo katika nchi za Chad, Pakistan na Yemen, ambako hakuna mabadiliko na
mwaka uliopita.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni