Jumatatu, 20 Oktoba 2014

MATUKIO YA UTEKAJI WA WATOTO NA MAUAJI YA WANAWAKE YANAENDELEA KUCHUKUA SURA MPYA

Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la mama Debora ameuwawa kwa kukatwa  mapanga yeye pamoja na watoto wake wawili na watu wasiojulikana huko Mkoani Bukoba na kufanya matukio ya utekaji wa watoto na kuuwawa kwa wanawake kushika kasi hapa nchini.

Kamanda wa polisi mkoani Bukoba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kutoa tamko kwa wananchi kwa ambao wanajiusisha na matukio kama haya watakapo kamatwa hawatakuwa na msamaha na kufuata sheria ili kuakikisha matukio haya hayawi endelevu.

Ni siku chache zimepita toka mwanamke mmoja kunyweshwa madawa ya kulevya na kuibiwa mtoto bado kuna matukio mengi yanaendelea kutokea ya kuibiwa kwa watoto ambao wamekuwa wakiuwawa na watu wasiojulikana na wengi wao kuibiwa.

Hata hivyo kamanda wa polisi mkoa wa Dar es salaamamewatoa hofu wananchi kwa amekanusha maneno ya watu yanayovuma ya kuwa wapo watu ambao wanatumia gari aina ya Noah na kuteka watoto na kuwataka wazazi kuwa walinzi wa watoto wao huku uchunguzi ukiendelea kufanyika kuhusu matukio hayo ambayo yanaendelea na kuwataka wazazi kuwaacha wototo waende shule.

DSC_0212

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni