Ijumaa, 24 Oktoba 2014

UNYAMA UNAOFANYWA NA WADADA WAKAZI ZA NDANI KWA WATOTO WAZIDI KUA TISHIO

Hausigeli aliyejulikana kwa jina moja la Ester (14) yupo matatani kwa madai ya kumuua mtoto Arafat Allan (3) kwa kumnyonga shingo na kumpiga na kitu kizito kichwani kisha kuutumbukiza mwili wake kwenye dimbwi la maji machafu,
Pichani ni mwili wa mtoto Alafat anayedaiwa kunyongwa kisha kutupwa kwenye dimbwi la maji
 Akizungumza kwa uchungu, mama mzazi wa mtoto huyo, Zakia Peter ambaye amelazwa katika Zahanati ya Kellen kutokana na mshtuko wa kifo cha mwanaye, alisema siku ya tukio, hausigeli huyo aliyekuwa na siku mbili tangu aanze kazi aling’ang’ania kutumwa sokoni saa mbili asubuhi ambapo alimkubalia na kumuagiza mboga.


Mama wa marehemu aliendelea kusema kuwa zoezi la kumsaka msichana huyo na mtoto wake liliendelea mpaka Jumanne iliyopita ambapo habari zilisambaa kwamba kuna maiti ya mtoto wa kiume imekutwa ikielea kwenye dimbwi la maji machafu linalotumika kumwagilia bustani za mboga maeneo hayo.

Mama wa mtoto akiwa ospitali baada ya kuzimia



Hili ni moja ya tukio ambayo yamekua yakilipotiwa yanayofanywa na wadada wakazi hii iwakumbushe wanawake wengine kuwa na hisporia nzuri ya wasichana wanowachukua ili kuepuka matatizo kama haya.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni